Kocha wa timu ya soka ya West Ham
United ya England Sam Allardyce amefichua mpango wake wa kuondoka
klabuni hapo hata kama timu hiyo ilimpa nafasi ya mkataba mpya.
Taarifa
za kuondoka kwa Allardyce zilitangazwa dakika za mwisho za mechi kati
ya West Ham dhidi ya Newcastle United, mtanange ambao uliisha kwa
ushindi wa bao mbili kwa bila walioupata Newcastle na kujinasua katika
janga la kushuka daraja. Allardyce ametumia miaka minne kuifundisha West
Ham lakini wagonga nyundo hao wameamua kutompa tena mkataba mpya katika
majira haya ya joto. "sikutaka kubaki, naweza sema kama tulikuwa
tunafikra sawa kama na wao hawakuwa wenye kunihitaji pia" alisema Kocha
huyo.
Hatimaye miamba ya soka nchini
Hispania Real Madrid imemtimua kocha wa timu hiyo Carlo Ancelotti baada
ya kuiongoza klabu hiyo kwa misimu miwili.
Kocha huyo raia wa
Italia, aliiongoza Madrid kutwaa taji la kombe la Hispania kabla ya
kuibebesha miamba hiyo taji la kumi la klabu bingwa barani Ulaya. Pamoja
na mafanikio hayo aliyoyapata msimu uliopita, mwaka huu haukuwa mzuri
kwa vijana hao wa Benabeu baada ya kuambulia patupu kwa kukosa hata
kombe moja japokuwa kikosi cha timu hiyo kinatajwa kuwa cha gharama ya
juu. Hasira za viongozi wa klabu hiyo ziliongezeka baada ya kutupwa nje
na Juventus katika hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa Ulaya huku
wapinzani wao wakubwa Barcelona ikinyakuwa taji la ligi kuu na kutinga
fainali ya klabu bingwa na kombe la Hispania. Rais wa Madrid Florentino
Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa haikuwa rahis kumtema kocha
huyo na kuongeza kuwa kocha mpya atateuliwa wiki ijayo.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza ameendelea na burudani ya kucheza
mpira mjini Bujumbura nchini humo.Huku maandamano ya raia kupinga
kugombea kwake awamu ya tatu yakiendelea nchini .Polisi wamekua wakizuia
maandamano hayo na kuuwawa baadhi ya raia.Hata hivyo rais huyo
ameonekana kutojali akiendelea na mambo yake.
Timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mchezo wake wa kwanza wa
kombe la COSAFA siku ya jumatatu dhidi ya Swaziland katika uwanja wa
Royal Bafokeng pembeni kidogo ya jiji la Rustenburg kuanzia majira ya
saa 1:30 jioni kwa saa za Afrika Kusini.
Awali
michezo ya kundi B ilikuwa ifanyike katika uwanja wa Olympia Park,
lakini waandaji wa michuano ya COSAFA Castle wamesema kutokana na sababu
zilizopo nje ya uwezo wao michezo hiyo imeshindikana kufanyika katika
uwanja huo.
Uwanja
wa Royal Bafokeng ni miongoni mwa viwanja viliyotumika katika Fainali
za Kombe la Dunia 2010 chini Afrika kusini, ukiwa na uwezo wa kubeba
watazamaji 42,000 huku timu ya Platinum Stars iliyopo Ligi Kuu
ikiutumia kama uwanja wake wa nyumbani.
Leo
asubuhi Taifa Stars imefanya mazoezi katika uwanja wa shule ya
Rustenburg chini ya kocha mkuu Mart Nooij, na wachezaji wote wapo katika
hali nzuri kuelekea katika mchezo huo wa jumatatu.
Kesho
jioni Taifa Stars ifanya mazoezi saa jioni katika uwanja wa Rolay
Bafokeng kwa ajili ya kuuzoea uwanja kabla ya mchezo wenyewe dhidi ya
Swaziland.
Akiongelea
hali ya hewa, kocha mkuu wa Taifa Stars Mart Nooij amesema vijana wake
wanaendelea kuizoea hali ya hewa, japokuwa kuna baridi hakuna mchezaji
aliyeshindwa kufanya mazoezi kutokana na hali ya hewa.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Barcelona’s
Lionel Messi from Argentina, centre left, scores his goal during a
Spanish La Liga soccer match between Real Madrid and FC Barcelona at the
Santiago Bernabeu stadium in Madrid, Spain, Sunday, March 23, 2014. (AP
Photo/Andres Kudacki)
Klabu za ligi kuu nchini Hispania zinatarajiwa kufanya mgomo mwishoni
mwa wiki hii ambapo hakutakuwa na michezo yoyote kufuatia kushindwa
kupatikana kwa makubaliano katika mkutano uliofanyika kati ya shirikisho
la wachezaji , uongozi wa ligi pamoja na shirikisho la soka la Hispania
.
Mgomo huu unakuja baada ya taarifa toka Serikalini ambayo iliarifu
juu ya kuwepo kwa makubaliano mapya ya mikataba ya televisheni ambapo
timu zote 20 zitaweza kufanya makubaliano ya mkataba wa haki za
matangazo ya televisheni kwa umoja na sio tofauti na klabu kubwa za Real
Madrid na Barcelona .
Umoja wa wachezaji unahisi kuwa bado matatizo yanayohusu malipo na
haki zao hayajapewa kipaumbele na hivyo kwa kauli moja wamekubaliana
kufanya mgomo ambao kimsingi utavuruga ratiba ya ligi ya Hispania .
Rais wa umoja wa wachezaji AFE Luis Rabes amethibitisha kuwa hakuna
muafaka uliofikiwa na pande zote katika kikao kilichofanyika hii leo
(jumanne) na kwa jinsi hali ilivyo hakutakuw ana michezo ya ligi ya
Hispania wikiendi hii .
Hata hivyo bado kuna nafasi ya hali hii kubadilika kwani pande zote
zinazohusika kwenye mazungumzo haya zitakutana katika mazungumzo mengine
hapo kesho na endapo muafaka utafikiwa basi huenda michezo ya mzunguko
wa 37 ikaendelea .
Hadi sasa Fc Barcelona ndio wanaongoza ligi na watajihakikishai
kutwaa ubingwa endapo watashinda mchezo wao dhidi ya Atletico Madrid
siku ya jumapili huku wakiwaacha mabingwa watetezi Atletico Madrid
wakishindwa kutetea ubingwa wao .
Mshambuliaji nyota wa timu ya Barcelona Luis Suarez atakuwa nje ya
michuano ya mataifa ya Amerika ya kusini maarufu kama Copa America
kutokana na kuendelea kutumikia adhabu ya kukosa michezo tisa kufuatia
kosa la kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chielini kwenye michuano ya
kombe la dunia mwaka jana .
Suarez atalazimika kuwatazama wenzie kwenye televisheni kutokana na
adhabu hiyo ambayo imebakiza michezo saba kabla ya kumalizika .
Uruguay inayofundishwa na kocha mkongwe Oscar Washington Tabarez
italazimika kumtegemea mshambuliaji wa PSG Edinson Cavani kwenye idara
ya ushambuliaji huku ikimkosa pia Diego Forlan ambaye amestaafu kucheza
timu ya taifa .
Forlan ambaye alistaafu mwezi machi mwaka huu amesema kuwa anaamini
Uruguay ina wachezaji wazuri na wenye uwezo ambao wataziba pengo la
Suarez na kufanya vizuri kwenye michuano ya mwaka huu .
Uruguay ndio mabingwa watetezi wa michuano ya Copa America ambayo
waliitwaa mwaka 2011 nchini Argentina ambako waliwafunga Paraguay kwenye
fainali na wanaingia kwenye michuano ya mwaka huu kama moja ya timu
zinazopewa nafasi ya kufanya vizuri
Miezi michache tu baada ya kumlaumu
mamake mzazi kwa kumroga na kumfanya apoteze fomu yake, Emmanuel
Adebayor anayeichezea timu ya Tottenham inayoshiriki ligi kuu ya soka
nchini Uingereza, amejitokeza na kufichua jinsi familia yake
ilivyomfanya afilisike bila shukrani.
Kupitia ukurasa wake wa facebook, Adebayor ameeleza kuwa
"Nimekuwa
nikiziweka taarifa hizi kwa muda mrefu lakini leo nimehisi kuwa ni
muhimu kuwaeleza nanyi pia. Ni kweli kuwa masuala ya familia hayastahili
kuwekwa hadharani lakini nafanya hivi ili familia nyingine nazo zipate
funzo kupita yaliyonisibu, Aliandika.
Anasema wakati alipokuwa na
umri wa miaka 17, aliutumia mshahara wake wa kwanza kuijengea familia
yake nyumba.Kama mnavyojua nilipokea tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika wa
mwaka, mwaka 2008.
Nilimpandisha mama yangu jukwaani kumshukuru
yeye kwa mambo yote. Mwaka ule ule nilimleta London kwa ajili uchunguzi
wa afya yake.
Wakati binti yangu alipozaliwa niliwasiliana na mama yangu kumweleza lakini alikata simu na sikujua ni kwanini.
Ukisoma
maoni yangu ya hivi karibuni watu wanasema mimi na familia yangu twende
tupate ushauri kwa muhubiri maarufu wa dini ya kikristo T.B Joshua.
Mwaka 2013 nilimpa mama yangu pesa ili aende kupata ushauri kwa mhubiri huyo nchini Nigeria.
Alipaswa
kukaa huko kwa wiki moja, lakini siku mbili tu alipofika nilipokea simu
kwamba ameondoka. Zaidi ya hayo nilimpa mama yangu pesa nyingi
kuanzisha biashara ya kupika chakula pamoja na bidhaa nyingine.
Kiuhalisia niliwaruhusu kuweka jina langu na picha yangu kwenye biashara hiyo ili waweze kuvutia wateja.
Ni kitu gani kingine mtoto wa kiume anaweza kufanya ndani ya uwezo wake kusaidia familia yake?
Miaka
kadhaa iliyopita, nilinunua nyumba huko East Lagon nchini Ghana kwa
dola milioni 1.2 za kimarekani. Nikaona ni vyema dada yangu mkubwa Yabo
Adebayor kuishi katika nyumba hiyo. Vile vile nilimruhusu kaka yangu
Daniel naye aishi kwenye nyumba hiyo.
Miezi michache baadae
nilifukuzwa kwenye nyumba niliyokuwa naishi ikianibidi kwenye hiyo
nyumba yangu. Kilichonishangaza niliona magari mengi kwenye barabara.
Kwa kweli dada yangu aliamua kuikodisha hiyo nyumba pasipo kunieleza.
Alimfukuza Daniel kwenye hiyo nyumba.
Mfahamu
kwamba nyumba hiyo ina vyumba 15. Nilipompigia dada yangu anipe
ufafanuzi alichukua karibu nusu saa kunishambulia na kunitukana kwenye
simu. Nilimpigia mama yangu anaelezee kisa kizima naye akafanya kama
dada yangu alivyofanya. Hivyo ni kama dada yangu alivyosema sina
shukrani.
Kaka yangu Kola Adebayor, anaishi nchini Ujerumani kwa
miaka ishirini na mitano sasa,safari zake zote za kurejea nyumbani mara
nne ametumia gharama zangu,kama hiyo haitoshi ninawasomesha watoto wake
na kuwalipia gharama zote kuhusiana na elimu yao.
Nilipokuwa
nchini Monaco ,alinifuata na kutaka pesa za kuanzishia biashra yake
.Mungu pekee ndiye ajuaye nilimpa kiasi gani cha kufungulia biashara
yake,kama ukimuuliza biashara hiyo iko wapi leo?
Masahibu
hayakuishia hapo,kaka yetu Peter alipoaga dunia nilimtumia Kola kiasi
kikubwa cha pesa ili arejee nyumbani,cha kushangaza hakutokea msibani
ama siku ya maziko.na leo kaka yule yule (Kola) anawaambia watu kuwa
chanzo cha kifo cha kaka yetu Peter ni mimi,linawezekanaje hili? Kaka
huyu huyu alikwenda kwenye gazeti la"The Sun" na kueleza habari za uongo
kuhusiana na familia yetu ili kujipatia fedha.
Wakatuma barua pia
katika klabu ya mpira ya Madrid nikafukuzwa.nilipokuwa nchini humo pia
nilipata wazo kuwa ni vyema kuwa na familia ya wana soka,hivyo
nikahakikisha kaka yangu Rotimi anajiunga na chuo cha mafunzo ya mpira
huko Ufaransa. Miezi michache tu,wachezaji ishirini na saba wa chuo hiyo
aliwaibia simu za mkononi wachezaji ishirini na mmoja .Sikuongea
chochote kuhusiana na kaka Peter Adebayor ,kwasababu hayuko nasi leo
hii,Mungu ailaze mahala pema peponi ,amina.
Dada yangu sasa, Lucia
Adebayor amekuwa na tabia ya kuwaambia watu kuwa baba yetu amenitaka
nimchukue dada huyu na kumpeleka ulaya,lakini sababu kubwa hasa ni nini
ya kumpeleka huko ulaya? Kila aliyeko hapa yupo kwa sababu.
Nilirejea
nyumbani Ghana nilipata taarifa za kaka yangu anaumwa sana,niliendesha
gari kwa kasi sana kuelekea Togo ili kukutana naye na kumpa msaada
anaostahili,nilipowasili huko mama yangu akanikatalia kumwona na
kunieleza kuwa ninachopaswa kufanya ni kumpa mama yangu pesa nay eye ata
maliza kila kitu.
Mungu pekee ndiye ajuaye siku ile ile
nikampatia mama yangu kiasi cha pesa alichokitaka,lakini cha ajabu watu
wanalalama kuwa sikufanya lolote kuokoa maisha ya kaka yangu Peter.je
mimi ni mpumbavu kiasi gani niendeshe gari mpaka Togo bure bila ya
sababu?
Nikaandaa mkutano wa kifamilia mwaka 2005 ili tumalize
tofauti zetu na matatizo yanayotuzunguuka.nilipowauliza maoni yao
wakanitaka kuwajengea nyumba kila mmoja wao na mishahara mikubwa kila
mwezi kwa kila mmoja wao.
Leo hii niko hai wamejimilikisha kila
kilicho change je nikifa itakuwaje?kwa sababu zote hizi,itanichukua muda
mrefu mno kuweka mikakati na misingi yangu barani Africa.kila wakati
ninajitahidi kuwasaidia wahitaji,familia yangu wao huhoji kila
nifanyacho na wote huona nimefanya uamuzi mbaya.
Ikiwa leo
ninaandika haya,sina lengo la kuwaanika watu wa familia yangu.ninataka
familia zingine za kiafrika kujifunza kutokana na ninayoyapitia mimi.
Asanteni sana