Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote

HATIMA YA JAMES LEMBELI KURUDI CCM HII HAPA ISOME.

Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli ambaye ni mwanachama wa Chadema mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano mjini Kahama mkoani Shinyanga.



Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli mara baada ya kuwasalimia wananchi waliofika kwa ajili ya kumsikiliza Rais katika viwanja hivyo vya Kahama.

Wakati jana Rais Magufuli akiwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga alimpa nafasi aliyekuwa Mbunge wa Kahama kwa tiketi ya CCM na baadae kuhamia CHADEMA, James Lembeli ili azungumze. 



Lembeli aliongea mambo kadhaa ikiwemo hatma yake kurudi CCM ambapo alisema yupo tayari kurudi iwapo Rais Magufuli atakisafisha chama kwa kuwashughulikia wanafiki na wala rushwa


Hapa chini ni maneno ya James Lembeli katika mkutano huo.
ANNA KILANGO AIBUKIA KANISANI NA KUTOA YA MOYONI BAADA YA KUTIMULIWA UKUU WA MKOA SHINYANGA

ANNA KILANGO AIBUKIA KANISANI NA KUTOA YA MOYONI BAADA YA KUTIMULIWA UKUU WA MKOA SHINYANGA

ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela, (Pichani) ameibukia kanisani na kutoa ya moyoni, ikiwa siku tano baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wake.

Kilango, ambaye Jumatatu wiki hii uteuzi wake ulitenguliwa baada ya Machi 20, mwaka huu, kudai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna mtumishi hewa wa serikali hata mmoja.

Hata hivyo, Ikulu ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa katika taarifa za awali kuna watumishi hewa 45, huku kazi ya uhakiki ikiendelea katika wilaya za Ushetu na Shinyanga.

Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wote, alipokuwa akiwaapisha kuwa wafanya uchunguzi kuhusu uwapo wa watumishi hewa katika mikoa yao na kutoa taarifa.

Kutokana na kutoa taarifa hizo zisizo za kweli, Jumatatu wiki hii, Rais Magufuli alitangaza kutengua uteuzi wake, akiwa amekaa kwenye nafasi hiyo kwa siku 27. Kilango amekuwa mkuu wa mkoa wa 19 tangu kuanzishwa kwa mkoa huo.

Mbali na Kilango, Rais Magufuli pia alimsimamisha kazi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Abdul Dachi, kutokana na taarifa hizo za kutokuwapo watumishi hewa katika mkoa.

ALIYOSEMA KANISANI
Akiwasalimia waumini wenzake juzi, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, mjini Shinyanga, baada ya kupewa fursa ya kusema neno, Kilango alisema anamshukuru Mungu kwa kila jambo kwa yote yaliyomtokea.

“Ndugu waumini wenzangu, hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu. Hata mtu unapojifungua mtoto akafariki dunia, unamshukuru Mungu kwani hayo ni mapenzi ya Mungu.

"Ukiona mzazi wako kafariki dunia pia, unamshuruku Mungu. Tunao wajibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema kwa maneno mafupi na kisha kuketi, huku akiacha simanzi miongoni mwa waumini wenzake, wakiwamo viongozi wa kanisa.

ALIVYOANZA KAZI
Mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), muda mfupi baada ya kuanza kazi, Kilango alisema Shinyanga ni mkoa wenye changamto nyingi ambazo atazishughulikia, lakini atakuwa akilazimika kukimbia Dar es Salaam kumwona mwenzi wake, Mzee John Malecela ambaye ni mgonjwa, na pindi hali yake ikiimarika wataungana naye mjini Shinyanga.

Hayo aliyasema Machi 22, mbele ya wajumbe wa kikao cha kamati hiyo na Ijumaa Machi 25, alisali kanisani hapo.

Sambamba na hayo, aliahidi kupambana na watumishi wazembe na wale wanaoendekeza rushwa na ufisadi na kurejesha hadi ya mkoa wa Shinyanga kimaendeleo.

Kilango ambaye yuko mjini Shinyanga, akisubiri kukabidhi ofisi kwa mrithi wake kwa mujibu wa utaratibu, bado anaishi hotelini kwa vile aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Ally Rufunga, hajaondoka katika nyumba ya serikali iliyoko Ikulu ndogo, eneo la Lubaga.

ALICHOKISEMA MAGUFULI
Wakati akipokea hundi ya Sh. bilioni sita kutoa kwa Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tilia Ackson, Rais Magufuli alisema aliwapa wakuu wa mikoa siku 15 wakasimamie watumishi hewa, ambazo zilimalizika Machi 31, mwaka huu.
Alisema katika siku hizo 15, aliwaruhusu kufanya kazi hiyo kwa uhuru na kuwaahidi hakutatokea kitu chochote na kwamba walifanya kazi vizuri.

Rais Magufuli alisema watumishi hewa waliopatikana ni 5,507 ambao walikuwa wanalipwa mishahara na miongoni mwao walikuwamo wanafunzi, waliokufa na waliofungwa.

Alisema serikali imekuwa ikitenga Sh. bilioni 583 kulipa mishahara na kati ya fedha hizo hulipwa watumishi hewa.
“Ninaamini uchambuzi utaendelea kufanyika ili kuokoa mabilioni ya fedha. Wizara ya Utumishi na ya Fedha muendelee kufanya kazi hiyo,” alisema Magufuli.

Alisema zaidi ya Sh. bilioni 53 zilikuwa zinapotea kwa kuwalipa watumishi hewa 5,507.

Rais Magufuli alisema watumishi hewa hawako katika halmashauri tu, bali wako kila idara ya serikali, zikiwamo Ofisi ya Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu, vyombo vya ulinzi na usalama, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na hata Wizara ya Fedha na Mipango.

Alisema wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa kwa kutambua tatizo hilo kuwa ni kubwa, aliwapa agizo hilo na wengi waliitikia wito na kufanya kwa ufanisi.

Rais Magufuli alisema akiwa wilayani Chato, aliona taarifa zikitolewa na wakuu wa mikoa kuhusu watumishi hewa, lakini alishangaa kusikia Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga (Kilango), akisema katika mkoa wake hakuna mtumishi hewa hata mmoja.

“Nilijiuliza ni kweli? Nikatoa maagizo nikiwa Chato kuwa watu waende 'ku-verify' (kuthibitisha) katika kila wilaya kama kweli hakuna watumishi hewa. Hadi jana usiku (Jumapili usiku) walipatikana watumishi hewa 45 na bado wilaya mbili zilikuwa hazijahakikiwa,” alisema.

“Niilijiuliza sana, nikajiuliza sana na kweli nilijuliza maswali mengi kwa masikitiko mengi kwa nini mkuu wa mkoa alizungumza vile wakati hakukuwa na adhabu yoyote, lengo lake lilikuwa nini?

“Je, kama ni mkuu wa wilaya au wasisidizi wake walimdanganya kwa nini na yeye alidanganya, ni shetani gani aliyemkumba? “Nimeamua nitengue uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga na atapangiwa kazi nyingine pamoja na katibu tawala wa mkoa,” alisema Maguful
MAGARI YAZIDI CHOMWA MOTO BURUNDI HALI BADO NI TETE.

MAGARI YAZIDI CHOMWA MOTO BURUNDI HALI BADO NI TETE.

.
Basi moja la uchukuzi limechomwa moto mjini Bujumbura Burundi na waandamanaji waliorejea mabarabarani kupinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Waandamanaji wanachoma moto magurudumu haswa katika eneo la Kanyosha.
Kitongoji hicho kimekuwa kitovu cha maandamano haya dhidi ya awamu ya tatu ya rais Nkurunziza.
.
Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura Ismael Misigaro amesema milio ya risasi inasikika mjini humo.
Maandamano haya yanarejea baada ya kuuawa kwa kiongozi wa chama cha upinzani Zedi Feruzi nje ya nyumba yake katika mji mkuu Bujumbura.
Aidha wanaharakati wa upinzani nchini humo wamesitisha mazungumzo na serikali rais Pierre Nkurunziza ya kutaka kutanzua mzozo ulioko wa kisiasa.
Wandamanaji wakienderea na uchomaji matairi ya gari.
.
Mzozo huo unafuatia hatua ya Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi ambao wengi wanasema kuwa unaenda kinyume na sheria na ndio iliyosababisha kuwepo kwa jaribio la kumpindua, na maandamano ya wiki kadhaa.
Tayari zaidi ya raia 100,000 wa taifa hilo wametorokea mataifa jirani.


UFISADI WAWAWEKA HATIANI WABUNGE WANNE KENYA.

UFISADI WAWAWEKA HATIANI WABUNGE WANNE KENYA.



Kiongozi wa Mashtaka ametoa ruhusa ya kushtakiwa kwa mwaziri wanne  
Kutumia ujumbe kwa vyombo vya habari, mkuu wa mashtaka ya umma nchini Kenya Keriako Tobiko, hii leo amevumbua yaliyomo katika hati za kesi za mawaziri wanne.
Tume ya maadili na kupambana na ufisadi ya Kenya imependekeza waziri wa uchukuzi mMhandisi Michael Kamau na waziri wa leba Kazungu Kambi kushtakiwa na matumizi mabaya ya ofisi.
Mhandisi Michael Kamau anakumbwa na shutuma za kutumia fedha ubadhirifu wa fedha za umma na kufanya mabadiliko katika ubunifu wa barabara ambayo tiyari ilikuwa imetengenezwa na mashauri.
Kazungu Kambi naye anadaiwa keteuwa wanachama wawili katika bodi ya shirika la taifa la hazina ya uzeeni kinyume na sheria.
Akizungumza na waandishi wa habari jana alasiri jumapili, afisa mkuu wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi Halakhe Waqo, alisema kwamba mawaziri wanne waliochunguzwa ni waziri wa Uchukuzi Mhandisi Michael Kamau, waziri wa ardhi, makao na ustawi wa miji bi Charity Ngilu, waziri wa kilimo Felix Kosgei, waziri wa leba Kazungu kambi, seneta wa Nairobi Mike Sonko na mbunge .
Tume hio imemwandikia rais Uhuru Kenyatta ombi la kuongeza muda wa uchunguzi wa kesi zilizobaki.
Siku sitini ambazo walikuwa wamepewa kukamilisha uchunguzi wa ripoti hiyo zimetimia leo.

Rais Uhuru Kenyatta alikuwa ametoa makataa ya siku 60 kushtakiwa kwa maafisa wakuu serikalini wafisadi
''Tumekuwa na shinikizo la kukamilisha kesi kwa wakati uliotolewa ila wajibu wetu wa kufanya uchunguzi wa kina ambao unaweza kustahimili uchunguzi mahakamani umetulazimu kuomba muda zaidi''alisema Halakhe Waqo
Kwa sasa tume hio imekamilisha kesi 56 kati ya 124 zilizowasilishwa kwa uchunguzi zaidi baada ya ripoti yao ya awali iliyokabidhiwa rais Kenyatta kuwasilishwa bungeni .
Kesi 21 tayari zimefikishwa kwa mkuu wa mashtaka ya umma Keriako Tobiko.
Kufikia sasa maafisa 19 wamefikishwa mahakamani na wengine 29, kulingana na afisa mkuu wa EACC, watafikishwa mahakamani siku chache zijazo katika maeneo kadhaa nchini yakiwemo Turkana, Machakos, Nyamira, Nairobi na Trans nzoia
Hata hivyo tume hii nayo pia imekumbwa na malumbano ya ndani kwa ndani ya shtuma za ufisadi, zilizosababisha kuchunguzwa kwa kiongozi wa tume hiyo na baadhi ya wanatume wake ambao hatimae walijiuzulu.

RATIBA YA URAISI CC YATOKA.WAGOMBEA KUSAKA WADHAMINIi 450, FOMU KUANZA KUTOREWA Juni 3


MGOMBEA Urais kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) atajulikana Julai 12 mwaka huu baada ya kukamilisha mchakato mzima wa kuomba kuwania nafasi hiyo, kutafuta wadhamini na kujadiliwa katika chama hicho.
 
Hayo yalielezwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari kueleza yanayoendelea katika siku ya pili ya kikao hicho mjini hapa.
 
Alisema mchakato wa kupata wagombea wa CCM katika vyombo vya dola yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, wabunge, wawakilishi na madiwani kwa uchukuaji wa fomu utafanyika kuanzia Juni 3 hadi Julai 15 mwaka huu.
 
Gharama za fomu hizo hazijapanda zimebaki vile vile kama zilivyokuwa mwaka 2010 na katika kanuni, yaani shilingi milioni 1 kwa urais, shilingi laki moja kwa ubunge na elfu hamsini kwa diwani.
 
Akifafanua zaidi alisema kwamba, wagombea Urais wataanza kuchukua fomu,bila mbwembwe kuanzia Juni 3 na kutakiwa kurejesha fomu hiyo mwisho saa 10 ya Julai 2 mwaka huu katika mazingira hayo hayo ya kutokuwepo na shamrashamra.
 
Aidha alisema kuanzia tarehe hiyo ya uchukuaji fomu hadi marejesho yake, wagombea watakuwa wanatafuta wadhamini 450 kutoka mikoa 15 nchini huku mikoa mitatu ikiwa ni kutoka Zanzibar na angalau mkoa mmoja uwe wa Unguja au kisiwa cha Pemba.
 
Ongezeko hilo la mikoa na wadhamini linatokana na haja ya kutafuta sampuli inayooana na idadi ya watu na mikoa kwa sasa. Tanzania ina mikoa 31.
 
Uchaguzi uliopita wagombea walitakiwa kutafuta wadhamini 250 katika mikoa 10, minane ikiwa ni kutoka Bara. Alisema wagombea urais hao wanapokwenda kutafuta wadhamini, wajumbe wote wa mkutano mkuu wa taifa hawataruhusiwa kuwa wadhamini, huku mwanachama atakayekuwa mdhamini akizuiwa kufanya udhamini wa zaidi ya mtu mmoja.
 
Kwa anayewania Urais wa Zanzibar tarehe za kuchukua na kurejesha ni zile zile za Jamhuri, huku akitakiwa kupata wadhamini 250 kutoka mikoa mitatu, mmoja ukiwa ama Unguja au Pemba.
 
Alisema vikao vya kuchuja wagombea Urais Zanzibar vitafanyika kuanzia Julai 4 hadi 10 ambapo Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM itamtaja Mgombea Urais wa Zanzibar.
 
Aidha wajumbe wote wa NEC hawaruhusiwi kumdhamini mgombea Urais wa Zanzibar. Akizungumzia fomu za wagombea Ubunge, alisema kwamba wanachama watachukua fomu hizo Julai 15 na kuzirejesha Julai 19 na mikutano ya kampeni itafanyika kuanzia Julai 20-31 ili kuomba kura.
 
Kura ya maoni ya kuwapata wanaowania nafasi ya Ubunge kupitia CCM itafanyika Agosti 1, mwaka huu. 
 
Kwa wanaowania Viti Maalumu ratiba ni ile ile, lakini safari hii mchujo wa mwisho utafanywa na Baraza kuu la UWT ambao kimsingi ndio wanaomiliki viti hivyo maalumu, ingawa mchujo wa awali utafanyika katika jumuiya husika.
 
Viti maalumu safari hii vitawaniwa pia na jumuiya ya wazazi ambao wamepewa viti viwili.Jumuiya nyingine ni jumuiya ya vijana, UWT yenyewe,jumuiya ya wasomi, wafanyakazi na wenye ulemavu.
 
Ratiba ya kuwania udiwani nayo ni Julai 15 hadi 19 na kura za maoni zitafanyika Agosti Mosi. Katibu huyo wa NEC hata hivyo aliwatahadharisha wanaowania nafasi hizo za dola kupitia CCM, kuangalia kwa makini kanuni za uchaguzi za chamhamshatz.blogsport.coma hicho, kuzisoma na kuzielewa kwa kuwa kama watafanya kosa litawagharimu ,huku akisisitiza ‘kosa moja goli moja’.
 
Akizungumzia namna ya kufanikisha kura ya maoni alisema chama chake kitafunga daftari la wanachama Julai 15 na wapiga kura wa chama hicho watalazimika kuwa na zaidi ya kadi ya chama kwa utambulisho ikiwamo kadi ya kupiga kura ili kushiriki kura ya maoni.
 
Alisema nia ya kuweka vitambulisho viwili ni kuzuia wapiga kura bandia ambao safari iliyopita walionekana kuwa chanzo cha matatizo. Aidha, wanafanya hivyo ili kuzuia wasioitakia mema CCM kula njama ya kuiangusha kupitia matumizi ya kadi bandia.
 
Aidha alisema ipo mikakati ambayo tayari inafanyiwa kazi kuhakikisha mchakato mzima hadi kura wa maoni unafanikiwa kuwapa Watanzania kile wanachokihitaji.
 
Pia alisema wagombea wote watakuwa pamoja katika mikutano ya kuomba kura. 
 
Akijibu swali maana ya maelekezo ya sasa kama ni hakikisho Katiba mpya haitakuwepo, Nape alisema CCM inafanya utaratibu wake kwa kuzingatia Katiba iliyopo sasa na kama katiba mpya itakuja watakutana kufanya mabadiliko yanayohitajika.

JIONEE MATUKIO MBALIMBALI YA MKUTANO WA CHADEMA ULIOFANYIKA JANA TANGANYIKA PACKERS KAWE Jijini Dar


Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA Mh.Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Parkers Jana, ambapo pia alizindua kitabu cha Mbunge wa jimbo la Kawe Mh. Halima Mdee.
 Mh Freeman Mbowe, Halima Mdee na John Mnyika wakizindua kitabu cha Mbunge wa Kawe Mh Halima Mdee
 Gwajima akiwa na baadhi ya viongozi wa CHADEMA
 Mchungaji Gwajima akiongozwa na Halima Mdee kwenye jukwaa kuu
 Wafuasi wa CHADEMA wakisikiliza hotuba ya mwenyekiti wao, Freeman Mbowe
Umati wa watu waliohudhuria mkutano wa CHADEMA uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers.

CHADEMA YARAHANI VIKALI SHERIA INAYO NYIMA UHURU VYOMBO VYA HABARI HAPA NCHINI.

Dk. Wilibroad Slaa akizungumzia juu sheria iyo mjini bukoba.hamshatz.blogsport.com

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewataka watanzania kuipinga na kutoikubali sheria  ya mpya iliyopitishwa ya takwimu kwa madai kwamba sheria hiyo inalenga kuzuia uhuru wa vyombo vya habari na kuwanyima watanzania haki na uhuru wa kupata habari.
 
Akihutubia hivi karibuni mjini Bukoba  katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk. Wilibroad Slaa alisema kupitishwa kwa sheria hiyo kunalenga kunyima uhuru wa habari pamoja na kuwafanya watanzania kuendelea kubaki gizani na kuishi kama wapo  shimoni bila kuelewa maovu yanayofanywa na viongozi wasio waadilifu wanaotumia madaraka vibaya kwa masalahi yao binafsi.
 
Alisisitiza kuwa  nia ya serikali kutaka kuzuia uhuru wa vyombo vya habari ni kuwarudisha nyuma watanzania ili waweze kuishi bila kupata habari kama ilivyokuwa enzi za ukoloni na kwamba hali hiyo haiwezi kuvumiliwa kwani serikali inataka kuficha maovu ambayo yanaweza   kuliangamiza taifa hapo baadae.

NAIBU KATIBU MKUU WA CCM -BARA,MWIGULU NCHEMBI AMEJIUZURU WADHIFA HUO KUTOKANA KUA ANATAKA KUGOMBEA WADHIFA MWINGINE.


Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba
----
Aliyekua Naibu Katibu Mkuu wa CCM -Bara,Mwigulu Nchemba amejiuzulu wadhifa huo.
 
Mwigulu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,ametangaza kujiuzulu nafasu hiyo  jana Jioni katika kikao cha Halmashauri Kuu ya ya Taifa ya CCM,Mjini Dodoma

Akithibiths tukio hilo,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi ,Naoe Nnauye amesema,Mwigulu ameamua kujiuzulu nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara kutokana na nia yake ya kutaka kuomba kuwania Urais kwa tiketi ya CCM  katika Uchaguzi utakaofanyika Octoba Mwaka huu

"Mwigulu alishamwambia nia hiyo Mwenyekiti wa Chama  Rais Jakaya Kikwete,nae Rais akamkubalia, na sasa  katika kikao ameomba rasmi kujiuzulu na Mwenyekiti Rais Jakaya Kikwete amemkubalia Mbele ya wajumbe wa NEC".amesema Nape

Nape amesema kufuatia uamuzi wa mwigulu  kujiuzulu, Mwenyekiti wa Chama Rais Jakaya Kikwete amemteua Msaidizi wake wa maswala ya siasa,Rajabu Ruhavi kuwa Mjumbe wa NEC na Wakati huohuo kamteua kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM -Bara Kushika nafasi iliyoachwa na Mwigulu Nchemb 
RAIS NKURUNZIZA AONGEA NA WAANDISHI KWA MARA YA KWANZA NA KUWATOLEA UVIVU AL-SHABAAB BAADA YA KUFELI KWA JARIBIO LA KUMPINDUA BURUNDI.

RAIS NKURUNZIZA AONGEA NA WAANDISHI KWA MARA YA KWANZA NA KUWATOLEA UVIVU AL-SHABAAB BAADA YA KUFELI KWA JARIBIO LA KUMPINDUA BURUNDI.

hamshatz.blogsport.comhttp://www.therwandan.com/ki/files/2012/08/nkurunziza.jpg
 
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amejitokeza kwa mara ya kwanza tangu jaribio la mapinduzi la jumatano iliyopita.

Rais Nkurunziza akihutubia waandishi wa habari katika ikulu ya Bujumbura alionya kuwa kuna tishio la shambulizi la kigaidi kutoka kwa kundi la waislamu kutoka Somalia wenye uhusiano na Al-Qaeda , Al Shabaab.

Aliwaambia wandishi wa habari wa kimataifa kuwa tishio hilo la mashambulizi sio tu kwa taifa lake bali pia kwa Kenya na Uganda .

Hata hivyo mwaandishi wa BBC aliyeko Bujumbura anasema kuwa Nkurunziza hakuzungumzia lolote kuhusu hali ilivyo nchini Burundi wala tishio la mapinduzi dhidi yake.
Wapinzani wake wanashuku ni njama ya kuidhinisha makabiliano makali na waandamani hapo kesho

Aliondoka ghafla akiwa mongoni mwa msafara uliolindwa kikamilifu.

Wapinzani wake hata hivyo wanasema huenda hiyo ni njama ya rais Nkurunziza kuidhinisha makabiliano makali dhidi ya wapinzani wake ambao tayari wameagiza wafuasi wao kujitokeza kwa wingi hapo kesho kuendelea na maandamano ya kumtaka asiwanie kipindi cha tatu katika kura za urais zitakazofanyika mwezi ujao.


Al Shabab wametishia kuishambulia Burundi kufuatia mchango wake katika majeshi ya AMISOM

Duru kutoka kwa afisi za maswala ya usalama wanje katika serikali ya Marekani na vile vile maswala ya ndani ya serikali ya Uingereza zimekariri tishio hilo la Al Shaabab dhidi ya Burundi kufuatia mchango wake katika jeshi la umoja wa Afrika Amisom huko Somalia.

Marekani tayari imeagiza raia wake kuondoka nchini humo kufuatia tishio la shambulizi la kigaidi mbali na kuzorota kwa hali ya usalama

WAUAJI WA ALBINO WANASWA BAADA YA KIGOGO WA CCM Mh MARAMPAKA KUNASWA NA VIUNGO VYA ALBINO IKIWA NI FUVU,MIKONO NA MIGUU.



Jeshi la polisi Mkoani Simiyu linamshikilia Chigila Gilala mkazi wa kijiji cha Bukigi kata ya Malampaka wilayani Maswa (45) kwa kosa la kukutwa na viungo zinavyodhaniwa kuwa vya binadamu likiwemo fuvu la kichwa.

Mtuhumiwa huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM katika kijiji hicho na Mganga wa tiba asili alikamatwa nyumbani kwake, baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa- alikuwa amewahifadhi majambazi kwa ajili kugangwa (kuzindikwa).

-Akitoa taarifa kwa waandishi wa kamanda wa -jeshi la polisi Mkoani Simiyu Gemini Mushy alieleza kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa mwenyekiti huyo lilitokea Mei 9 mwaka huu -majira ya saa 11 jioni katika kijiji hicho.


Jeshi la polisi Mkoani Simiyu linamshikilia Chigila Gilala mkazi wa kijiji cha Bukigi kata ya Malampaka wilayani Maswa (45) kwa kosa la kukutwa na viungo zinavyodhaniwa kuwa vya binadamu likiwemo fuvu la kichwa.

Mtuhumiwa huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM katika kijiji hicho na Mganga wa tiba asili alikamatwa nyumbani kwake, baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa- alikuwa amewahifadhi majambazi kwa ajili kugangwa (kuzindikwa).

-Akitoa taarifa kwa waandishi wa kamanda wa -jeshi la polisi Mkoani Simiyu Gemini Mushy alieleza kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa mwenyekiti huyo lilitokea Mei 9 mwaka huu -majira ya saa 11 jioni katika kijiji hicho.


ll


Kamanda Mushy alisema kuwa askari wakiongozwa na mkuu wa upelelezi katika wilaya ya Maswa walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuwepo kwa majambazi nyumbani kwa mganga huyo, kuwa alikuwa amewahifadhi kwa ajili ya kuwazindika.

Alisema baada ya kupata taarifa hizo walifanya msako nyumbani kwa mwenyekiti huyo, ambapo- alibainisha kuwa walianza kufanya upekuzi ndani na nje ya nyumba.

“Wakati wakifanya upekuzi huo walikutana na mfuko wa sandarusi ukiwa chini ya lundo la kuni nje ya nyumba- ya mwenyekiti huyo..na katika mfuko huo kulipatikana fuvu la kichwa pamoja na mifupa ya mikono au miguu vinavyodhaniwa kuwa ni viungo vya binadamu” Alisema Mushy.

Kamanda alieleza kuwa jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi kama kweli viungo hivyo ni vya binadamu na kama anahusika na uwepo wa viungo hivyo kutokana na -kukutwa nje ya nyumba yake.


Wakati huo huo kamanda Mushy alibainisha kuwa jeshi hilo linamshikilia- Gandula Mashimo mkazi wa kijiji cha Longalombogo kata ya Migato wilaya ya Itilima Mkoani hapa kwa kukutwa na Bunduki ya kivita SMG na risasi 273.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi majira ya saa 3:30 usiku kijijini hapo, akiwa embeba siraha hiyo pamoja na risasi katika mfuko wa sandarusi.

Alisema mtuhumiwa alikamatwa baada ya wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wilayani humo, ambapo alikamatwa akiwa njiani kuelekea kusikojulikana.

-
Mushy alieleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini washirika wake, ikiwemo na matumizi ya silaha hiyo, huku akitoa wito kwa wananchi mkoani hapa kutoa taarifa za watu wanaowahisi kuwa siyo wema katika maeneo yao.

Aidha alitoa onyo kwa ambaye anamiliki silaha bila kibali rasmi, kuwa ajisalimishe pamoja na silaha yake mara moja kabla ya msako mkali kuanza.

Rasmi Kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Aifariji Familia ya Nyerere


J

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo leo asubuhi nyumbani kwa Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye John Nyerere kilichotokea hivi karibuni.Aliyesimama pembeni ya Rais ni mdogo wa marehemu Makongoro Nyerere.
.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia ya marehemu John Nyerere nyumbani kwao Msasani jijini Dar es Salaam leo asubuhi. 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye John Nyerere kilichotokea juzi .Mwili wa Marehemu John Nyerere rubani wa zamani wa ndege za kivita nchini aliyeshiriki kikamilifu vita vya Uganda kati ya mwaka 1978 na 1979, unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda kijijini Butiama mkoani Mara kwa maziko.Picha na Freddy
Taarifa kamili ya jinsi Kajala alivyopigwa chupa usiku night club Dar es salaam.

Taarifa kamili ya jinsi Kajala alivyopigwa chupa usiku night club Dar es salaam.

kajala 2
May 11 2015 Kajala akionekana na jeraha lake juu ya jicho la kushoto kwenye meza ya Majaji wa shindano la vipaji Kinondoni Dar es salaam.
May 10 2015 mwigizaji wa bongomovie Kajala amekwenda kumsupport msanii Mabeste ambaye alifanya show New Maisha Club kwa ajili ya kuchangisha pesa za kumsaidia mke wake kwenye matibabu.
Kajala anasema''Mpaka tumemaliza show, sasa kwenye muda wa kuondoka nikamwambia Meneja wangu amuite msanii wetu mmoja anaitwa Tausi ili tuondoke, sasa wakati nataka kushuka kwenye gani natembea tu sijui chochote nikashangaa chupa imenipiga usoni, nikadondoka na kubiringika kwenye zile ngazi, kuna mkaka na mdada wakaniona wakanisaidia"
Kajala 1
‘Aliyenipiga na hiyo chupa ni Mwanaume, simjui na wala sijawahi kumuona hata mara moja…. amekamatwa yuko Osterbay Polisi, nilivyotoka Maisha Club nilipelekwa Hospitali Mwananyamala nimeshonwa usoni aliponiumiza, tukarudi Polisi nikaandika maelezo‘ Kajala
Kwenye sentensi nyingine Kajala amesema ‘Huyu Mwanaume aliulizwa pale Polisi anasema eti ni Pombe, lakini mtu eti Pombe umeingizwa ndani saa moja tu unakumbuka kwamba ni pombe ndio imekufanya hivyo? sio kweli….. itakua tu alidhamiria yeye mwenyewe’
Unaweza kumsikiliza Kajala akiongea yote mengine kuhusu hili tukio kwa kubonyeza play hapa chini….
YANAYOJIRI LEO BUNGENI DODOMA

YANAYOJIRI LEO BUNGENI DODOMA

 
  
April 15, 2014, Muungano bado kasheshe 
Kikao cha Bunge maalum la katiba kinaendelea leo hii, kinachojadiliwa hasa ni sura ya kwanza na sita ya Rasimu ya Katiba. 


Kama ilivyo kawaida, wajumbe wanaendelea kulumbana, Chama Cha Mapinduzi wakikazania Muundo wa serikali mbili na wale wa upinzani wakitetea serikali tatu, kama ilivyowasilishwa na Tume Maalum ya kukusanya maoni iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.

Wajumbe wa Bunge hilo kutoka Zanzibar, ambao ni muhimu sana kwa ajili ya upatikanaji wa Katiba hii, kwa kuwa ni lazima theluthi mbili wakubali ili kupitisha kipengele chochote, wanaendelea kuvutana, juu ya serikali mbili au tatu huku pia wakipigana vijembe.
Zifuatazo ni baadhi ya kauli zilizosisimua kutoka kwa baadhi ya wajumbe


Mh. Mbaruku: Anaunga muundo wa serikali mbili maana ndiyo anaamini utawapa Zanzibar utajiri na Zanzibar itakuwa Half London.

Mh. Hija Hassan Hija: Anasema watanganyika hawana hasara ya serikali mbili wala moja maana walishachukua mali zote kwa miaka 50 iliyopita na Zanzibar wameibiwa kwa miaka 50 iliyopita. Zanzibar ilipwe kwa muda huo.

Anasema wenye mali ni Tanganyika, mawaziri wa Zanzibar wamekuwa wakisema muungano umekuwa ukiwaonea na anashangaa ni nini kimewapata. Anasema kuna mawaziri wana maslahi yao ndo maana wanashindwa kuipigania Zanzibar.
Anasema hawatetei muungano bali wanatetea maslahi yao maana kuna watu walikuwa wanapigania muungano ila baada ya kupewa uwaziri wakakaa kimya kwa hiyo hawa ni wasaka tonge, wana njaa.

 Mh. Pamela Masai: Anasema wajumbe wameacha maslahi yenye tija kwa watanzania wote na kukimbilia kwenye muundo wa serikali.
Anaunga mkono maoni ya wachache kwenye Kamati namba 10. Na anaunga mkono Lugha ya kiswahili kutumika kama lugha ya taifa.
Anapinga vipengele vya Uadilifu, uwajibikaji uwazi na usawa kuondoshwa kweye tunu ya taifa.
Anasema kamati zote zimeunga mkono sura ya pili ibara ya sita 2(6), anasema kwa hiyo hata mamlaka waliyonayo wajumbe wa BMK ni mamlaka waliyopewa wananchi.
Anapendekeza muundo wa Serikali tatu. Anasema kama wananchi wanataka serikali mbili basi waendelee na serikali tatu alafu wananchi wapendekeze maoni ya muundo wa serikali wanayotaka.

Mh. Mwinyi Haji Makame: Anasema muungano huu waasisi wetu wameleta muungano wa undugu na sio vinginevyo.
Gari ya serikali mbili ishachemka na haizuiliki, anasema hata wakina Jussa wakileta unafiki na chuki muundo huu utaendelea kuwepo..
Anasema miaka 50 ya Mapinduzi ndiyo umeijenga Zanzibar.
Anamalizia kwa kusema kuwa matatizo ya Zanzibar kwa muundo huu wa serikali mbili yashashughulikiwa ndani ya kamati zote zilizoundwa kutatua matatizo ya wazanzibar.

Mh. Chiku Abwao: Anaanza kwa kusema yeye ni muumini wa muungano na muungano wa shirikisho ndiyo utaondoa muungano wa manung'uniko na kuhakikisha Tanganyika inapatikana kwa gharama yoyote, ananukuu ''Jasiri ni yule anayejali kwao''
Anasema bora muungano uvunjike ila Tanganyika ibaki na anaunga muundo uliopendekezwa na tume ya Warioba maana ni maoni ya wananchi walio wengi.
Anamnukuu Lukuvi kuhusu jeshi kutawala nchi kama muundo wa serikali tatu ukipita na kusema hata hivyo jeshi lipo kwa ajili ya wananchi wa Tanzania pia anawasifu wazanzibar kwa kupigania utaifa wao.
Anasema wabunge walio wengi wa tanzania hawapo bungeni kuunga muungano wa tanganyika na zanzibar bali wapo kuunga mkono muungano wa TANU na AFRO-SHIRAZI Party.

Mh. Oluoch: Anasema kumbe bungeni ni sehemu ambapo ukweli unaachwa na uongo kuchukuliwa. Anasema hata waasisi waliunganisha mchanga wa Tanganyika na Zanzibar ili kuunda serikali moja na sio mbili kama ilivyo sasa.
Anasema ikiwa wazanzibar wakitaka muungano hawatapiga kura ya kuunga muundo wa serikali mbili...
Anasema walimu wanaunga hoja serikali tatu.

Shamsa Mwangunga: Anatoa pongezi kwa serikali ya JMT kwa kulea muungano huu mpaka kufikia miaka 50 maana malezi yanapitia changamoto nyingi.
Anasema muungano huu ni tunu maana nchi nyingi zimejaribu kuwa na muungano na shirikisho ila hawakuweza kufika mbali ila kwa muungano huu wa Tanzania ni suala la kujivunia kuwepo mpaka sasa hivi. Uvumilivu na upendo wa watanzania ndo umeleta muungano huu kuwa imara na kero mbali mbali zimeweza kutatuliwa na kubaki kero moja ya uchumi.
Utawala bora tumekuwa tukisifiwa duniani kwa kuwa na utawala bora kwa kuweza kuudumisha muungano huu na kuna watu wamekuwa wakipotosha kuwa kuna kero wakati sio kweli hakuna kero na kero zilizobaki ni ndogo na zinafanyiwa kazi.
Anasema serikali ya nchi mbili ni zimwi tulijualo na tumelizoe na serikali ya nchi tatu hatulijui ''Zimwi likujualo halikuli likakwishaaaa''

Mh. Salehe Nassoro Juma: Msimamo wake ni muungano wa serikali tatu na anawatoa wasiwasi watanzania na wapemba wanaofanya biashara ya vitunguu tanzania bara kuwa serikali tatu hazivunji muungano na kama ukivunjika tanzania imesaini mkataka wa haki za binadamu na wataendelea kuishi kama DIASPORA hata muungano ukivunjika.
Anamshukuru mh. Kikwete kwa kuanzisha mchakato huu wa katiba mpya, maana kabla ya mchakato huu ilikuwa kosa la jinai kuzungumzia muundo wa muungano.
Anasema hakuna asiyejua kuwa muundo wa serikali mbili una tatizo na suluhisho la matatizo haya ni muundo wa serikali tatu, anasema pia kuwa mawazo ya waasisi wetu yamezeeka inabidi yafanyiwe modification na ametolea mfano wa China jinsi walivyofanyia modification mawazo ya waasisi wao na mambo yanaenda vizuri.

Mh. Haji Omar: Anaanza kwa kuunga mawazo aliyoyatoa kwenye kamati no 7 mawazo ya walio wengi kwenye sura ya 1 & 6 juu ya muundo wa serikali mbili.
Uhalai wa Karume kuchukua dhamana ya watu wa Zanzibar kuhusu muungano, anasema mzee Karume alikuwa anatimiza ilani ya chama chake cha ASP juu ya umoja na kuhakikisha elimu, matibabu yanakuwa bure na makazi bora kwa wazanzibar wote.
Faida za muungano, anasema
1.Umeme jimbo la Tumbatu
2. -Anasema wananchi walio wengi Zanzibar wanaunga muundo wa serikali mbili.

Mh. Ezekiel Maige: Anasema kuwa lugha zinazotolewa na Wazanzibari zina ukakasi. Anasema kuwa Zanzibar ina wilaya 10 ambazo zote zina barabara za lami na umeme tofauti na Tanzania Bara.
Anasema kuwa hayo yote hawayaoni na badala yake wanazidi kulalamika kuwa wanaonewa na Bara. Anahoji iwapo ikatokea Zanzibar kukawa na utajiri mkubwa kuliko Bara, je Wazanzibari watakuwa tayari kuisaidia Bara?

Mh. Fahmi Dovutwa: Alama za taifa zitakua wimbo wa taifa, nembo ya taifa na bendera. Dola haimtambui Mungu kwa hiyo wimbo wa taifa itolewe kwenye alama ya taifa. dhana ya kuomba Mungu asaidie ina maana dola haifungamani na dini. Nami ntasimama nitapigana kuhakikisha Katiba inamtambua Mungu.
Kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine. Sera ya TANU iliruhusu wazee watoto na walemavu kunyonya. Nataka iwe kutegemeana sio kunyonyana.
Watu wanaoamini serikali tatu mpaka sasa wameshindwa kutuonesha jinsi watakavyotatua matatizo tulio nayo. watu wa serikali tatu wameshindwa kujenga hoja. Namlaumu sana Mbowe. Chadema wana serikali za majimbo lakini wanashindwa kufafanua vizuri.
Natoa shukrani za pekee za Rais kwa kuridhia hii ijadiliwe na kusimamia elimu za kata. Namshukuru pia Lowasa aliye mshauri Rais.

Mh. Joseph Mbilinyi: Naunga mkono serikali tatu kama ilivyoletwa na Tume ya katiba, kwa hiyo tunaunga mkono maoni ya wananchi.
Aliyeharibu huu mchakato ni Rais aliyekuja kuelezea msimamo wa chama chake badala ya kuzindua bunge.
Hiki ni kipindi cha Kwaresma acheni unafiki. Tumeharibu pesa nyingi. CCM wameishiwa mikakati wameanzisha mkakati wa kuzomea. Mwingulu anataka serikali moja lakini anaogopa kusema. Tuko kwenye nafasi nzuri sana la kujadili hili suala la sivyo tutalijadili kwa kulazimishwa.

Leo Lukuvi anatutishia nchi itatawaliwa na jeshi, vizuri, mbona Rais wetu alikua mwanajeshi na anatuongoza? wanajeshi ni ndugu zetu, wakitawala kuna tatizo gani?

Serikali tatu ni tija. kila chenye gharama kina faida. Mara nyingi viongozi wa dini wanakosea wanapokuwa upande wa dola dhidi ya wananchi. Mfano Rwanda. Unapopima malaria au ukimwi inapimwa kwenye kidole sio mwili mzima acheni kuzingua eti waliohojiwa ni wachache.


Kategori

Kategori