Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote

HATIMA YA JAMES LEMBELI KURUDI CCM HII HAPA ISOME.

Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli ambaye ni mwanachama wa Chadema mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano mjini Kahama mkoani Shinyanga.



Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli mara baada ya kuwasalimia wananchi waliofika kwa ajili ya kumsikiliza Rais katika viwanja hivyo vya Kahama.

Wakati jana Rais Magufuli akiwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga alimpa nafasi aliyekuwa Mbunge wa Kahama kwa tiketi ya CCM na baadae kuhamia CHADEMA, James Lembeli ili azungumze. 



Lembeli aliongea mambo kadhaa ikiwemo hatma yake kurudi CCM ambapo alisema yupo tayari kurudi iwapo Rais Magufuli atakisafisha chama kwa kuwashughulikia wanafiki na wala rushwa


Hapa chini ni maneno ya James Lembeli katika mkutano huo.
ANNA KILANGO AIBUKIA KANISANI NA KUTOA YA MOYONI BAADA YA KUTIMULIWA UKUU WA MKOA SHINYANGA

ANNA KILANGO AIBUKIA KANISANI NA KUTOA YA MOYONI BAADA YA KUTIMULIWA UKUU WA MKOA SHINYANGA

ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela, (Pichani) ameibukia kanisani na kutoa ya moyoni, ikiwa siku tano baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wake.

Kilango, ambaye Jumatatu wiki hii uteuzi wake ulitenguliwa baada ya Machi 20, mwaka huu, kudai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna mtumishi hewa wa serikali hata mmoja.

Hata hivyo, Ikulu ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa katika taarifa za awali kuna watumishi hewa 45, huku kazi ya uhakiki ikiendelea katika wilaya za Ushetu na Shinyanga.

Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wote, alipokuwa akiwaapisha kuwa wafanya uchunguzi kuhusu uwapo wa watumishi hewa katika mikoa yao na kutoa taarifa.

Kutokana na kutoa taarifa hizo zisizo za kweli, Jumatatu wiki hii, Rais Magufuli alitangaza kutengua uteuzi wake, akiwa amekaa kwenye nafasi hiyo kwa siku 27. Kilango amekuwa mkuu wa mkoa wa 19 tangu kuanzishwa kwa mkoa huo.

Mbali na Kilango, Rais Magufuli pia alimsimamisha kazi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Abdul Dachi, kutokana na taarifa hizo za kutokuwapo watumishi hewa katika mkoa.

ALIYOSEMA KANISANI
Akiwasalimia waumini wenzake juzi, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, mjini Shinyanga, baada ya kupewa fursa ya kusema neno, Kilango alisema anamshukuru Mungu kwa kila jambo kwa yote yaliyomtokea.

“Ndugu waumini wenzangu, hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu. Hata mtu unapojifungua mtoto akafariki dunia, unamshukuru Mungu kwani hayo ni mapenzi ya Mungu.

"Ukiona mzazi wako kafariki dunia pia, unamshuruku Mungu. Tunao wajibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema kwa maneno mafupi na kisha kuketi, huku akiacha simanzi miongoni mwa waumini wenzake, wakiwamo viongozi wa kanisa.

ALIVYOANZA KAZI
Mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), muda mfupi baada ya kuanza kazi, Kilango alisema Shinyanga ni mkoa wenye changamto nyingi ambazo atazishughulikia, lakini atakuwa akilazimika kukimbia Dar es Salaam kumwona mwenzi wake, Mzee John Malecela ambaye ni mgonjwa, na pindi hali yake ikiimarika wataungana naye mjini Shinyanga.

Hayo aliyasema Machi 22, mbele ya wajumbe wa kikao cha kamati hiyo na Ijumaa Machi 25, alisali kanisani hapo.

Sambamba na hayo, aliahidi kupambana na watumishi wazembe na wale wanaoendekeza rushwa na ufisadi na kurejesha hadi ya mkoa wa Shinyanga kimaendeleo.

Kilango ambaye yuko mjini Shinyanga, akisubiri kukabidhi ofisi kwa mrithi wake kwa mujibu wa utaratibu, bado anaishi hotelini kwa vile aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Ally Rufunga, hajaondoka katika nyumba ya serikali iliyoko Ikulu ndogo, eneo la Lubaga.

ALICHOKISEMA MAGUFULI
Wakati akipokea hundi ya Sh. bilioni sita kutoa kwa Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tilia Ackson, Rais Magufuli alisema aliwapa wakuu wa mikoa siku 15 wakasimamie watumishi hewa, ambazo zilimalizika Machi 31, mwaka huu.
Alisema katika siku hizo 15, aliwaruhusu kufanya kazi hiyo kwa uhuru na kuwaahidi hakutatokea kitu chochote na kwamba walifanya kazi vizuri.

Rais Magufuli alisema watumishi hewa waliopatikana ni 5,507 ambao walikuwa wanalipwa mishahara na miongoni mwao walikuwamo wanafunzi, waliokufa na waliofungwa.

Alisema serikali imekuwa ikitenga Sh. bilioni 583 kulipa mishahara na kati ya fedha hizo hulipwa watumishi hewa.
“Ninaamini uchambuzi utaendelea kufanyika ili kuokoa mabilioni ya fedha. Wizara ya Utumishi na ya Fedha muendelee kufanya kazi hiyo,” alisema Magufuli.

Alisema zaidi ya Sh. bilioni 53 zilikuwa zinapotea kwa kuwalipa watumishi hewa 5,507.

Rais Magufuli alisema watumishi hewa hawako katika halmashauri tu, bali wako kila idara ya serikali, zikiwamo Ofisi ya Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu, vyombo vya ulinzi na usalama, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na hata Wizara ya Fedha na Mipango.

Alisema wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa kwa kutambua tatizo hilo kuwa ni kubwa, aliwapa agizo hilo na wengi waliitikia wito na kufanya kwa ufanisi.

Rais Magufuli alisema akiwa wilayani Chato, aliona taarifa zikitolewa na wakuu wa mikoa kuhusu watumishi hewa, lakini alishangaa kusikia Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga (Kilango), akisema katika mkoa wake hakuna mtumishi hewa hata mmoja.

“Nilijiuliza ni kweli? Nikatoa maagizo nikiwa Chato kuwa watu waende 'ku-verify' (kuthibitisha) katika kila wilaya kama kweli hakuna watumishi hewa. Hadi jana usiku (Jumapili usiku) walipatikana watumishi hewa 45 na bado wilaya mbili zilikuwa hazijahakikiwa,” alisema.

“Niilijiuliza sana, nikajiuliza sana na kweli nilijuliza maswali mengi kwa masikitiko mengi kwa nini mkuu wa mkoa alizungumza vile wakati hakukuwa na adhabu yoyote, lengo lake lilikuwa nini?

“Je, kama ni mkuu wa wilaya au wasisidizi wake walimdanganya kwa nini na yeye alidanganya, ni shetani gani aliyemkumba? “Nimeamua nitengue uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga na atapangiwa kazi nyingine pamoja na katibu tawala wa mkoa,” alisema Maguful
MAGARI YAZIDI CHOMWA MOTO BURUNDI HALI BADO NI TETE.

MAGARI YAZIDI CHOMWA MOTO BURUNDI HALI BADO NI TETE.

.
Basi moja la uchukuzi limechomwa moto mjini Bujumbura Burundi na waandamanaji waliorejea mabarabarani kupinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Waandamanaji wanachoma moto magurudumu haswa katika eneo la Kanyosha.
Kitongoji hicho kimekuwa kitovu cha maandamano haya dhidi ya awamu ya tatu ya rais Nkurunziza.
.
Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura Ismael Misigaro amesema milio ya risasi inasikika mjini humo.
Maandamano haya yanarejea baada ya kuuawa kwa kiongozi wa chama cha upinzani Zedi Feruzi nje ya nyumba yake katika mji mkuu Bujumbura.
Aidha wanaharakati wa upinzani nchini humo wamesitisha mazungumzo na serikali rais Pierre Nkurunziza ya kutaka kutanzua mzozo ulioko wa kisiasa.
Wandamanaji wakienderea na uchomaji matairi ya gari.
.
Mzozo huo unafuatia hatua ya Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi ambao wengi wanasema kuwa unaenda kinyume na sheria na ndio iliyosababisha kuwepo kwa jaribio la kumpindua, na maandamano ya wiki kadhaa.
Tayari zaidi ya raia 100,000 wa taifa hilo wametorokea mataifa jirani.


UFISADI WAWAWEKA HATIANI WABUNGE WANNE KENYA.

UFISADI WAWAWEKA HATIANI WABUNGE WANNE KENYA.



Kiongozi wa Mashtaka ametoa ruhusa ya kushtakiwa kwa mwaziri wanne  
Kutumia ujumbe kwa vyombo vya habari, mkuu wa mashtaka ya umma nchini Kenya Keriako Tobiko, hii leo amevumbua yaliyomo katika hati za kesi za mawaziri wanne.
Tume ya maadili na kupambana na ufisadi ya Kenya imependekeza waziri wa uchukuzi mMhandisi Michael Kamau na waziri wa leba Kazungu Kambi kushtakiwa na matumizi mabaya ya ofisi.
Mhandisi Michael Kamau anakumbwa na shutuma za kutumia fedha ubadhirifu wa fedha za umma na kufanya mabadiliko katika ubunifu wa barabara ambayo tiyari ilikuwa imetengenezwa na mashauri.
Kazungu Kambi naye anadaiwa keteuwa wanachama wawili katika bodi ya shirika la taifa la hazina ya uzeeni kinyume na sheria.
Akizungumza na waandishi wa habari jana alasiri jumapili, afisa mkuu wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi Halakhe Waqo, alisema kwamba mawaziri wanne waliochunguzwa ni waziri wa Uchukuzi Mhandisi Michael Kamau, waziri wa ardhi, makao na ustawi wa miji bi Charity Ngilu, waziri wa kilimo Felix Kosgei, waziri wa leba Kazungu kambi, seneta wa Nairobi Mike Sonko na mbunge .
Tume hio imemwandikia rais Uhuru Kenyatta ombi la kuongeza muda wa uchunguzi wa kesi zilizobaki.
Siku sitini ambazo walikuwa wamepewa kukamilisha uchunguzi wa ripoti hiyo zimetimia leo.

Rais Uhuru Kenyatta alikuwa ametoa makataa ya siku 60 kushtakiwa kwa maafisa wakuu serikalini wafisadi
''Tumekuwa na shinikizo la kukamilisha kesi kwa wakati uliotolewa ila wajibu wetu wa kufanya uchunguzi wa kina ambao unaweza kustahimili uchunguzi mahakamani umetulazimu kuomba muda zaidi''alisema Halakhe Waqo
Kwa sasa tume hio imekamilisha kesi 56 kati ya 124 zilizowasilishwa kwa uchunguzi zaidi baada ya ripoti yao ya awali iliyokabidhiwa rais Kenyatta kuwasilishwa bungeni .
Kesi 21 tayari zimefikishwa kwa mkuu wa mashtaka ya umma Keriako Tobiko.
Kufikia sasa maafisa 19 wamefikishwa mahakamani na wengine 29, kulingana na afisa mkuu wa EACC, watafikishwa mahakamani siku chache zijazo katika maeneo kadhaa nchini yakiwemo Turkana, Machakos, Nyamira, Nairobi na Trans nzoia
Hata hivyo tume hii nayo pia imekumbwa na malumbano ya ndani kwa ndani ya shtuma za ufisadi, zilizosababisha kuchunguzwa kwa kiongozi wa tume hiyo na baadhi ya wanatume wake ambao hatimae walijiuzulu.

Kategori

Kategori